Tuesday, July 12, 2016

PICHA 6 : DC wa Korogwe alivyobeba tofali baada ya shule kubaki na darasa moja tu lililo salama

June 30 2016 ilikuwa siku  ya mwisho ambayo Rais Dk John Pombe Magufuli aliitoa kwa wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya kumaliza tatizo la madawati lililokuwa linasumbua kwa miaka mingi kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari kukaa chini.

Baada ya baadhi ya mikoa kumaliza tatizo hilo kwa asilimia kubwa lipo pia tatizo la kuchakaa na upungufu wa madarasa jambo lililomfanya mkuu wa wilaya ya Korogwe Gabriel Robert kuingia mtaani kusaidiana na wananchi kujenga madarasa matatu kati ya saba ambayo yanahitajika katika shule ya msingi Makondora.

Kilichofanya Mkuu wa wilaya na wananchi kuingia site ni baada ya shule hiyo kubaki na darasa moja ambalo ni salama na mengine ni hatarishi kwa wanafunzi na kuta zinaweza kudondoka wakati wowote.


 Mkuu wa wilaya ya Korogwe Gabriel Robert


Kikundi cha kinamama LIMCA kiliposikia na kuona juhudi za DC kilijitokeza na kutoa mifuko 15 ya Cement. 





 

No comments:

Post a Comment