Tuesday, July 12, 2016

Msami: Sina uhusiano na Kajala, ila ikitokea ni poa tu

Msanii wa muziki na mwalimu wa dance, Msami Giovani amesema kuwa haoni kama kuna tatizo lolote endapo akiwa yupo kwenye mahusiano na staa wa filamu Bongo, Kajala Masanja. 


Muimbaji huyo amekiambia kipindi cha E-News cha EATV, “Sioni kama kuna ubaya mimi kutoka na Kajala.” 

“Sijasema nina mahusiano na Kajala ila ikitokea tukawa wapenzi tunaweza kuzungumza mimi na yeye kujua hatima yake na mume wake ambaye anatumikia kifungo kwa sasa,” ameongeza.

Masami na Kajala wamekuwa wakionekana wakiwa pamoja mara nyingi hali ambayo imeibua maswali kwa mashabiki kuwa huenda wawili hao wakawa wanatoka kimapenzi.
Hata hivyo hadi sasa ni Quick Rocka ndiye anajulikana kama mpenzi wa Kajala.

No comments:

Post a Comment