Na sasa mwandishi wa hit ya Rihanna na Drake, Work, PARTYNEXTDOOR amedai kuwa awali aliuandika wimbo huo kwa lengo la kumpa Rihanna, lakini label yake haikuupenda na hivyo alifikiria kumpa Alicia Keys.
“Label yake [Rihanna] haikuwa inajali kuhusu muziki wa Caribbean wakati huo,” aliliambia The New York Times na kuongeza kuwa kidogo aamue tu kukaa nayo kabla ya kufikiria kumpa Alicia Keys. Mwisho wa siku alisema Rihanna aliupigania.
PARTYNEXTDOOR anadai Rihanna alimwambia kuwa Work ni wimbo unaopendwa zaidi na familia yake.
Work ni wimbo uliofanywa vizuri kwenye chati duniani ikiwa ni pamoja na kukaa kwenye chati ya Billboard kwa muda mrefu.
No comments:
Post a Comment