Muongozaji huyo amekiambia kipindi cha Planet Bongo cha EA Radio kuwa hawezi kufanya kazi na kampuni ya Wanene kwa kuwa na yeye anamiliki kampuni yake.
“Hizo ni story tu sijafanya kazi na Wanene, sijawahi kufanya kazi na Wanene na sifanyi nao kazi kwa sababu mimi nina kampuni yangu inajitegemea,” amesema Msafiri.
“Sijasaini mkataba kwamba nafanya kazi na Wanene na wala Wanene hawajasaini na mimi,” ameongeza.
Msafiri ni mmoja kati ya waongozaji wenye uwezo mkubwa kwa sasa ndani ya Bongo ambao video anazotengeneza zinafanya vizuri kwenye TV tofauti tofauti.
No comments:
Post a Comment