Friday, August 19, 2016

Burna Boy atangaza kustaafu muziki,Lily Allen amtolea uvivu

Msanii wa miondoko ya Dancehall kutoka nchini Nigeria Burna Boy, usiku wa Jumatano hii, August 17, kupitia ukurasa wake wa Twitter, aliwashangaza mashabiki wake kwa kutangaza kuwa ataacha muziki baada ya tamasha lake litakalofanyika mjini London October 1.
Burna Boy aliandika ujumbe huu ‘Thinking of quitting music for real after d 1st of October maybe.’ Mashabiki wengi walishangazwa na uamuzi huo wa Burna boy wa kuamua kustaafu kufanya mziki mapema.
Lakini Wapo pia mashabiki wengine waliomkejeli Burna Boy kuwa anatafuta kiki zisizo na mpango ili tu kuipromote show yake hiyo. Burna Boy alionekana kukasirishwa na baadhi ya majibu ya mashabiki zake waliokuwa wakimkejeli.
Vile vile Mwimbaji wa kimataifa kutoka Uingereza Lily Allen amemtolea uvivu Burna Boy kuhusu kolabo yao wanayoitarajia kuitoa. Lily Allen alimtumia ujumbe huu Burna Boy ‘@ burnaboy that’s a shame . I was gonna finish our song next week.
Lily Allen

Burna Boy hakukaa kimya na alimjibu Lily Allen kwa maneno haya ‘u know I ain’t going no where man! They don’t even know the amount of waves coming thru!! Can’t wait!!’ the ‘Yawa Dey’.
Muda mfupi baadaye Burna Boy aliwapunguza kidogo presha mashabiki zake kuhusu mustakabali wake wa kustaafu kwa mfululizo wa tweets wenye ujumbe huu
‘I wud quit if it was just me
but I got bruddas that’s Died for this
n I got pple who took their undying
love for me n my music to d grave.’
‘My 1/10/16 concert in London wud b
a great way to say goodbye tho. On d
contrary it will only b d beginning of
new levels unlocked! # Powers’





No comments:

Post a Comment